Deuteronomy 16:5-8

5Kamwe msitoe dhabihu ya Pasaka katika mji wowote ambao Bwana Mwenyezi Mungu wenu amewapa, 6 aisipokuwa mahali atakapopachagua kama makao kwa ajili ya Jina lake. Hapo ndipo lazima mtoe dhabihu ya Pasaka jioni, jua litakapotua, iwe kumbukumbu yenu ya kutoka Misri. 7 bOkeni na mle mahali pale ambapo Bwana Mwenyezi Mungu wenu atakapopachagua, kisha asubuhi mrudi kwenye mahema yenu. 8 cKwa siku sita mtakula mikate isiyotiwa chachu na siku ya saba fanyeni kusanyiko kwa ajili ya Bwana Mwenyezi Mungu wenu na msifanye kazi.

Sikukuu Ya Mavuno

(Kutoka 34:22; Walawi 23:15-21)

Copyright information for SwhKC